HYAC

Attack with Style, Defend with Heart

Saturday 30 November 2013

WATANZANIA WAWILI KUKIMBIA PUNE INTERNATIONAL MARATHON DESEMBA MOSI



Michuano ya Pune (Poona) International Marathon inatarajiwa kufanyika kesho Jumapili (Desemba Mosi 2013) nchini India, huku Tanzania ikiwakilishwa na wanariadha wawili tu kutoka katika Klabu ya Holili Youth Athletics.
 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari mapema leo mchana imesema wanariadha hao ambao walianza safari yao Novemba 27, mwaka huu ni Oswald Revelian Kahuruzi ambaye anashiriki mbio hizo kwa mara ya 3 na Pascal Mombo Sarwat ambaye ni mara yake ya kwanza kushiriki mbio hizo.

Rais wa Holili Youth Athletics Domician Rwezaura alisema Oswald Kahuruzi atakimbia mbio hizo katika umbali wa Kilometa 42 wakati Sarwat atakimbia Half Marathon ambayo ni Kilometa 21.

Blogu hii ilifanya mahojiano nao majira ya saa 3:35 asubuhi kwa saa za Afrika Mashariki kwa saa za India ilikuwa ni saa 6:35 mchana kuhusu mustakabali wao katika mbio hizo hasa ikizingatiwa wao ni watanzani a pekee wanaoipeperusha bendera.

Kwa pamoja wanaraidha hao walisema changamoto ni kubwa kutokana na ukweli kwamba hali ya hewa kwa sasa katika mji huo ni joto hivyo watajitahidi kuipeperusha bendera.

Hata hivyo walibainisha kuwa nchi mahiri duniani kwa kutoa wanariadha ambazo ni Ethiopia na Kenya zimeleta wanariadha wengi ikilinganisha na Tanzania.

Ethiopia imewaleta wanariadha 100 na Kenya ikiwa na wanariadha 48.
Itakumbukwa kwamba Pune ni mji ulio karibu kabisa na Jiji Mahiri nchini India la Mumbai.

No comments:

Post a Comment