HYAC

Attack with Style, Defend with Heart

Wednesday 26 March 2014

NELSON MRASHAN AHITIMU MAFUNZO YA UKOCHA RIADHA TANZANIA


NELSON MRASHANI

Nelson Brighton Mrashan ni miongoni mwa makocha wa mchezo wa Riadha waliohitimu mafunzo ya ukocha ngazi ya pili ya cheti.

Nelson Mrashan alihitimu mafunzo hayo Machi 28, mwaka huu, yaliyochukua majuma mawili kuanzia Machi 15 hadi 28 mwaka huu Mjini Kibaha.

Akizungumza baada ya kuhitimu mafunzo Mrashan alisema huo ni mwanzo mzuri katika kuinua mchezo wa riadha nchini Tanzania.

Chama cha Riadha nchini kimetoa shukrani zake za dhati kwa Holili Youth Athletics Club (HYAC) kuwa mbele katika kuinua mchezo wa riadha hasa ikizingatiwa kuwa Nelson Mrashan ni Operation Manager wa klabu hiyo.

RT kupitia barua yake kwa HYAC ya Machi 28 mwaka huu ilisema wahitmu wa mafunzo hayo wanapaswa kupewa kipaumbele katika kutambuliwa kwao ili waweze kutoa taaluma waliyoipata na sio kukaa na vyeti bila kuwajibika
WAHITIMU WA MAFUNZO YA UKOCHA MJINI KIBAHA MACHI 28, 2014


Tuesday 18 March 2014

RAIS KIKWETE MGENI RASMI SOKOINE MINI MARATHON 2014



Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika msimu wa pili wa mbio za Sokoine zitakazofanyika katika Kijiji cha Monduli Juu, wilaya ya Monduli, mkoani Manyara, kama sehemu ya maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 30 ya kifo cha aliyekuwa Waziri mkuu wa Tanzania, hayati Edward Moringe Sokoine.
Rais Kikwete anatarajiwa kuwasili wilayani Monduli ambapo pia atahudhuria ibada maalum ya kumbukumbu itakayofanyika katioka kanisa la Monduli Juu na baadae kushuhudia mbio zitakazofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Monduli Juu.
Akizungumza na Waandishi wa Habari, Mratibu wa Mbio hizo, Wilhelm Gidabuday alisema maandalizi yam bio hizo zitakazofanyika April 12, tayari yameshaanza na kuongeza kuwa kila kitu kinakwenbda sawa kama ilivyokuwa imepangwa.
“Mgeni Rasmi mwaka huu ni Rais Kikwete, tumeshafanya mawasiliano yote na tunaamini mwaka mbio zitafana na kubeba sura ya Utaifa, mwaka jana tulimwalika Rais lakini kutokana na majukumu alishindwa kuhudhuria, lengo letu ni kuhamasisha umoja na uzalendo na sio njaa,” alisema Gidabuda. 
Gidabuday alisema yake imeamua kumwalika kiongozi huyo mkuu wan chi kutokana na Heshimaaliyonayo Marehemu Sokoine katika historia ya Taifa hili na kuongeza kuwa lengo la kuandaa mbio hizo kama ilivyokuwa mwakja jana ni kumbapo pia kutakuwa na watu na viongozi mbalimbali.
Gidabuday alisema kutokana na changamoto  zilizojitokeza mwaka jana, kamati8 yake imejipanga vyema kuhakikisha mbio hizo zinakuwa moja ya mashindano makubwa yanayoandaliwa katika ardhi ya Tanzania ukiacha mbio za Kilimanjaro Marathon zilizofanyika hivi karibuni mjini Moshi.
“Tumejiweka sawa, mbio za mwaka jana zilituachia mengi ya kujifunza na kwa mwaka huu tunaamini tumejifunza na tuko tayari kuwapa Watanzania burudani ya kweli, niseme tu kwamba mwaka huu tumelenga kufanya mabadiliko makubwa sana ukianza na zawadi kwa washindi,” alisema Gidabuday.
Aidha Gidabuday alisema zaidi ya wanariadha pamoja na watu mbalimbali mashuhuri wakiwemo wabunge na Viongozi mbalimbali wakuu wa nchi tayari wameshajitokeza na kuthibitisha kushiriki mbio hizi ambazo lenge lake ni kuhamasisha uzalendo na mshikamano.
Baadhi ya waliomba mpaka sasa ni wanafuzni wapatao 200 kutoka katika shule za msingi na Secondari katika maeneo ya jirani na Kijiji cha Monduli Juu mbio zitakapofanyikia, wanariadha wazoefu akiwemo mshindiu wa mwaka jana kilomita 21, Dickson Marwa kutoka Klabu ya Riadha ya Holili, Holili Youth Athletic Club (HYAC).
Gidabuday aliwataja wengine kuwa ni pamoja na watu wazima ambao mpaka sasa wameshafikia 50 ambapo  kwa mwako huu jumla ya washiriki zaidi ya 1000 wanatarajiwa kushiriki.

Imeandikwa na Fadhil Athuman, Monduli-Arusha

HYAC YAJITOSA UDHAMINI SOKOINE MINI MARATHON 2014



K
labu ya Holili Youth Athletics Club (HYAC) ya mjini Holili, mkoani Kilimanjaro, imejitosa kudhamini mbio za Sokoine Mini Marathon zinazotarajiwa kufanyika Aprili 12, mwaka huu katika Kijiji cha Monduli Juu, Wilaya ya Monduli, mkoani Arusha.


Domician Genandi, 
Managing Director 
(HYAC).
Katika udhamini huo, HYAC imetoa sh milioni moja zitakazotumika kuchapisha namba (Bibs), 1,000 za utambulisho za wanariadha.

Akizungumza na vyombo vya habari Mkurugenzi wa HYAC, Domician Genandi, alisema kilichomsukuma kufanya hivyo ni moyo wa uanamichezo na kuongeza kuwa, kwa mwaka huu wamedhamiria kuongeza nguvu zote kuinua mchezo wa Riadha nchini.

“Nimeamua kusaidia nikiwa kama mdau, sababu lengo letu ni kuendeleza michezo Tanzania, sisi wadau tunatakiwa tuwe na mtazamo wa ushindi kama taifa na si ushindi wa klabu zetu binafsi tu, au wanariadha wetu tu, HYAC tunatambua jitihada binafsi zinazofanywa na waandaaji kumuenzi hayati Sokoine,” alisema Genandi.

Aidha, Genandi alisema kwa mwaka huu klabu yake inatarajiwa kushirikisha wanariadha wengi zaidi, ambako lengo lake ni kuhakikisha anaendeleza rekodi ya mwaka jana.

Hata hivyo Mkurugenzi huyo alitaka Sokoine Mini Marathon ifanyike siku moja kabla ya tukio ili wanariadha nao wapate muda wa kuhudhuria maadhimisho ya mkongwe huyo kisiasa hapa nchini hasa ikizingatiwa kwamba maadhimisho hubeba vitu vingi.

Pia Domician alitanabaisha siku moja kabla inainua uchumi wa eneo husika hivyo siku zinapokuwa chache hufanya uchumi kukua taratibu kutokana na ukweli kwamba maadhimisho hayo hukusanya washiriki wengi kila mwaka.
Kwa upande wake, Mratibu wa mbio hizo, Wilhelm Gidabuday alisema kwa udhamini huo HYAC inakuwa klabu ya kwanza ya riadha hapa nchini kudhamini mashindano yanayoandaliwa na wadau wengine wa riadha na kuongeza kuwa, katika hilo wameonesha kweli kwamba wana nia nzuri ya kuendeleza michezo hapa nchini hasa riadha.