HYAC

Attack with Style, Defend with Heart

Thursday 24 April 2014

ELIBARIKI BUKO, WAMURA LAMECK KUCHUANA MBIO ZA KUADHIMISHA MIAKA 50 YA MUUNGANO WA TANZANIA



Wanariadha wawili kutoka Holili Youth Athletics Club wanatarajiwa kukimbia mbio fupi katika kuadhimisha miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibari Jijini Dar es Salaam siku ya Jumamosi.


Wanariadha hao ni Elibariki Buko na Wambura Lameck ambao watakimbia mbio za mita 800 na 1500

Itakumbukwa kuwa Elibariki Buko alikimbia Sokoine Min Marathon 2014 kilomita 10 ikiwa ni sehemu yake ya kujipanga vizuri kuelekea kuadhimisha miaka 50 ya Muungano wa Tanzania, na kushika nafasi ya 17 kati ya wanariadha 200.

Wambura Lameck ana rekodi ya kufanya vizuri katika mashindao ya kimataifa hasa ikizingatiwa kwa mara ya kwanza kushiriki michuano ya kimataifa ilikuwa ni mwezi Machi mwaka huu nchini Uganda akishika nafasi ya 16 katika kilomita 8 kati ya wanariadha 150 walioshiriki mbio hiyo.

Wambura Lameck anatarajiwa mwanzoni mwa mwezi ujao kutua nchini Sweden kwa michuano ya kimataifa akiwa ni miongoni mwa wanariadha kutoka nchini Tanzania.

Mkurugenzi Mtendaji wa Holili Youth Athletics Club, Domician Genandi amesema anatarajia kuona vijana wake wakifanya vizuri katika mbio hizo kwani wana vipaji vinavyoweza kuufanya mchezo wa riadha kutazamwa kama ilivyokuwa mika ya 1960.

Imetolewa na:
Jabir Johnson
Afisa Habari, Holili Youth Athletics Club
+255-(0)-768 096 793

No comments:

Post a Comment