HYAC

Attack with Style, Defend with Heart

Friday 30 January 2015

HOLILI YOUTH YASHIRIKI UZINDUZI KILI MARATHON 2015, MOSHI



 Director de Holili Juventud Atletismo Club (HYAC) Domician Genandi, llega a Palacio de Kibo para inaugration Maratón de Kili 2015. 


Klabu ya Riadha ya Holili Youth (HYAC) imeshiriki katika shughuli za uzinduzi wa mbio za Kili Marathon mwaka huu katika viunga vya Kibo Palace Home mjini Moshi jana ikiongozwa na mkurugenzi wa klabu hiyo Domician Genandi.

Ujumbe wa watu 8 kutoka klabu hapo uliwasili katika viunga vya Kibo Palace Home ambapo Mgeni rasmi alikuwa Katibu Tawala mkoa wa Kilimanjaro Severin Kahitwa akimwakilisha mkuu wa mkoa.

Holi Youth (HYAC) ilikaribishwa na baada ya hafla hiyo kumalizika waliwekea mkanda uliokuwa ukielezea ushiriki wa klabu hii katika kuinua vipaji  vya riadha hapa nchini na ushiriki wao katika Kili Marathon mwaka uliopita.

Wadhamini wa Mbio hizo mwaka huu ni Kilimanjaro Premier Lager ambapo wanadhamini kilometa 42, Tigo kilometa 21 na GAPCO wanamichezo wasiojiweza, wenye mahitaji maalum.
Kibo Palace Home inamilikiwa na Laswai miongoni mwa wafanya biashara maarufu mkoani Kilimanjaro.














No comments:

Post a Comment