HYAC

Attack with Style, Defend with Heart

Thursday 15 January 2015

PASCALINA SYVESTER KUJIUNGA NA HOLILI



PASCALINA SLYVESTER (KUSHOTO) AKIWA NA MWALIMU JAMBAU AMBAYE ALIKUWA AKIMNOA AKIWA SINGIDA



Mwanariadha Chipukizi Pascalina Slyvester (17) kutoka Singida anatarajiwa kujiunga na wanariadha wengine wa Holili Youth Athletics Club (HYAC) katika mazoezi ya kujiandaa na michuano mbalimbali mwaka huu.

Nyota huyo chipukizi wa mbio fupi na za kati alionwa na klabu hiyo katika mbio za Rotary Marathon 2014 Jijini Mwanza alipotimua mita 1500.

Klabu ya riadha ya Holili Youth inaendelea na kampeni zake za kutafuta vipaji vya riadha nchini kwa maendeleo ya mchezo wenyewe na taifa kwa ujumla.

Pascalina atajiunga katika kambi ya mazoezi ya Holili iliyopo wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro.
 PASCALINA SLYVESTER AKIKABIDHIWA TUZO BAADA YA KUMALIZIA WA TATU KATIKA KARATU SPORTS FESTIVAL 2014 MKOANI ARUSHA


















No comments:

Post a Comment