HYAC

Attack with Style, Defend with Heart

Friday 15 August 2014

KONA YA PRO, JULAI 2014: GENANDI AITAKA JAMII YA KITANZANIA KUJIPANGA MASHINDANO MAKUBWA YA RIADHA



 Julai 2014
Yaliyomo
  1. UTANGULIZI
  2. HOLILI YOUTH ATHLETICS CLUB
  3. UNAWAKUMBUKA?
  4. AFYA NA RIADHA
  5. SURPRISE RIO!
  6. B’E
  7. TO THE BEST
  8. BIOGRAPHY CHAMBER
UTANGULIZI
Baada ya pilikapilika za Kombe la Dunia nchini Brazil mwezi Juni na Julai mwaka huu sasa tumekutana tena huku tukiwa na mengi ya kuzungumza katika Utangulizi wetu kwenye toleo hili.

Michuano ya Jumuiya ya Madola imemalizika katika Jiji la Glasgow nchini Scotland huku watanzania tukiishia patupu katika michezo mitano iliyokwenda kutuwakilisha.

Nijikite katika mchezo wa riadha, ambao umetupa masikitiko makubwa, kwani tulijua kwamba hatutachukua medali yoyote kutokana na mfumo wa uteuzi wa wachezaji wetu.

Kubwa zaidi tusahau yaliyopita kwani viongozi wetu wamerudi wakiwa vichwa chini kutokana na wachezaji waliowateua  kuiwakilisha Tanzania katika michuano hiyo kufanya vibaya.

Licha ya kwenda na kurudi bila medali yoyote lakini ninajua wazi kuwa kuna mambo viongozi wetu wa Chama cha Riadha (RT) na Kamati ya Olimpiki (TOC) watakuwa wamejifunza huko, rai yangu kwao ni kwamba mambo hayo mazuri waliyoyaona na kuyapata huko wawarudishie watanzania kwani “kuvunjika kwa koleo sio mwisho wa uhunzi”.

Wachezaji hawatakiwi hata kidogo kuacha kufanya mazoezi kwani itatugharimu zaidi katika michuano ijayo, hivyo basi ni wazi kujifunza na kurekebisha pale tulipokosea ili kutulia katika msemo usema “Don’t live in the past, Learn from it…”

Nikutakie utendaji mwema wa majukumu yako kwa mwezi Agosti.
Domician Genandi
Mkurugenzi Mtendaji
Holili Youth Athletics Club (HYAC)
Julai 2014.

No comments:

Post a Comment