HYAC

Attack with Style, Defend with Heart

Friday 7 February 2014

RAIS KIKWETE YAITE MAKAMPUNI KUWEKEZA KATIKA RIADHA



Miaka ya 1980, nchini Kenya wakati huo Rais wa nchi hiyo alikuwa ni Daniel Arap Moi ambaye alikuwa akitawala akipokea madaraka kutoka kwa Mtangulizi na Mwasisi wa Taifa hilo Jomo Kenyatta.
 
Alichokifanya Moi aliutazama mchezo wa riadha nchini mwake na kuona kwamba unahitaji kufanyiwa mabadiliko ya hali ya juu ili kuiwezesha nchi hiyo kufanya vizuri kimataifa.

Aliyaita makampuni mawili akayaambia yauwezeshe mchezo huo kupanda kwa kiasi kikubwa, makampuni hayo mara baada ya kupewa rai hiyo yalianza kazi mara moja na ndio Kenya unayoiona hii leo ikifanya vizuri katika mchezo huo.

Kumekuwa na ubishani kwamba siasa haitakiwi katika michezo kwani ikiingia itasababisha madhara makubwa na hata michezo yenyewe isifanikiwe.

Lakini leo nasema “Siasa ndio kila Kitu” lakini je inatekelezwaje katika medani ya michezo.

Tumekuwa tukipiga kelele kuhusu mchezo wa riadha katika nchi ya Tanzania tangu enzi za kina Filbert Bayi, Suleiman Nyambui na wengineo waliandika historiakatika riadha ya Tanzania.

Moi aliongea tu na makampuni mawili tu na mambo yakenda vizuri, sasa inashindikanaje kwetu Tanzania ambako hakika tumejaliwa kuwa na hazina ya kila kitu.

Tulichokosa katika riadha yetu  nimaamuzi ya kiongozi wetu mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa mwenye hadhi ya kimataifa  Jakaya Mrisho Kikwete.

Sio lazima mheshimiwa Rais useme na vyombo vya habari tuje ila ni muhimu ukiona vyema kuita vyombo vya habari, kubwa zaidi ni kuyaita makampuni nchini kuwekeza katika Riadha.

Mheshimiwa Rais, binafsi nakupenda sana kutokana na uwezo wako wa kuweza kushawishi katika mambo mbalimbali, sasa ningekuomba ufanye na hili na kama ujuavyo muda wako wa kukaa madaraka ndio huo unapunga mkono.

Nimemzungumzia Moi kwasababu katika riadha alithubutu kufanya licha ya udhaifu wake katika serikali wakati ule hadi alipotolewa na Mwai Kibaki kupitia NARC, wakenya wanamkumbuka kwa hilo.

Kwako Kikwete ni muhimu ukafanya hivyo licha ya kutuletea Kombe la Dunia, UEFA Champions League kuzuru nchini lakini kumbuka jambo moja kwamba riadha ndio mchezo pekee ulileta medali nchini Tanzania.

Napolean Hill katika kitabu chake cha “Think, and Grow Rich” anaandika  kwamba ukiweza kufikiria katika mwono sahihi, utajiri utakuja pasipo mashaka.

Robert Kiyosaki katika kitabu chake cha “Cashflow Quadrant”  anasema kuwekeza katika masuala fulani husababisha maendeleo katika jamii husika, lakini hiyo inawataka watu wanajua nini maana ya kuwepo ulimwenguni.

Haina haja ya maandamano kuja kwako ikulu kukushinikiza Mheshimiwa Rais kuongea na makampuni maana wewe ndio mpini wa Tanzania hakuna wa kuleta “fyoko fyoko” ukishasema, Baba Sema Basi!!!! Wanao wazalendo wa Tanzania tujivunie Utaifa wetu.

Imeandikwa na Johnson Jabir, Columnist

No comments:

Post a Comment