HYAC

Attack with Style, Defend with Heart

Monday 10 February 2014

RIADHA HARD TALK 2014 YAFANYIKA MOSHI




KATIBU WA CHAMA CHA RIADHA TANZANIA (RT) SULEIMAN NYAMBUI AKISISITIZA JAMBO

MOSHI: (JAIZMELALEO) - Mjadala wa wazi kuhusu riadha nchini Tanzania “RIADHA HARD TALK 2014”  ulioandaliwa na Holili Youth Athletics Club (HYAC) ya mkoani Kilimanjaro umefanyika jana Februari 9, mwaka huu huku ikibainika wachezaji na makocha wamekuwa wakiilalamikia serikali na Chama cha Riadha (RT) kutokana na elimu zao kuwa za kiwango cha chini.
 





Akizungumza katika mjadala huo uliofanyika mjini Moshi, Katibu Mkuu wa RT, Suleiman Nyambui alisema kwa takribani miongo miwili kumeibuka tabia ya watanzania wakiwemo makocha na wachezaji wa mchezo huo kuilalamikia serikali na RT kutowekeza vya kutosha katika riadha.

Nyambui alisema serikali imekuwa ikilalamikiwa kuwa haitaki kuwekeza katika mchezo wa riadha, wakati huo huo RT nayo ikilalamikiwa kwa kutosimama imara.

“Tuwe wakweli mbele za Mwenyezi Mungu na atutazame sasa, inakuwaje watanzania, makocha na wachezaji kulalamika kila kukuchapo kuhusu mchezo wa riadha lakini kinachoonekana uvivu wa kufikiri na kiwango cha elimu kuwa duni kwa watanzania ndio kimesababisha lawama kwa serikali na RT” alisema Nyambui.

Hata hivyo Nyambui aliwataka makocha na wachezaji kuacha kutupa lawama kwa serikali na RT kutokana na ukweli kwamba wengi wao hawataki kuongeza viwango vyao vya elimu hali inayosababisha wawe waoga katika kutoa maoni yao.

“ Ukiwa umesoma hautakuwa mwoga katika kutoa maoni yako mahali husika kwa hekima na busara, kama ni kocha utakuwa ukifundisha kwa weledi tofauti na ilivyo sasa ambapo makocha wenye sifa za kufundisha mchezo huo wapo wachache hata wengine kugeuka kuwa madebe matupu yaliapo upepo ukivuma” aliongeza Nyambui.

No comments:

Post a Comment