HYAC

Attack with Style, Defend with Heart

Monday 23 June 2014

BAGAMOYO HISTORICAL MARATHON 2014 YAFANYIKA


Wanariadha Ismail Juma na Jackline Sakilu wametwaa taji la mbio za kihistoria za “Bagamayo Half Marathon 2014” zilizofanyika mjini Bagamoyo mwishoni mwa juma.
ISMAIL JUMA, MSHINDI WA MBIO ZA KILOMETA 21
ASUBUHI YA JUNI 22, 2014 BAGAMOYO
Ismail Juma (Arusha) na Jackline Sakilu (JWTZ-Arusha) walitwaa taji hilo wakikimbia kilometa 21 kwa muda wa saa 1:03.20; 1:06.53 kila mmoja.

Kwa wanaume, Dickson Marwa alishika nafasi ya pili akikimbia kwa muda wa saa 1:03.27 huku Elia Daudi kutoka Dodoma akishika nafasi ya tatu akitumia muda wa saa 1:03.58.

Kwa wanawake, Failuna Abdi (Arusha) alishika nafasi ya pili akitumia muda wa saa 1:12.26, nafasi ya tatu ikishikwa na Zakia Mrisho (Arusha) akikimbia kwa muda wa saa 1:13.07.

Kwa upande wao Holili Youth Athletics Club (HYAC) katika mbio hizo za kilometa 21  kwa wanawake mwanadada pekee aliyekimbia mbio hizo Furaha Sambeke alishika nafasi ya 7 akikimbia kwa muda wa saa 1:20.40 akimpita Banuelia Brighton aliyeshika nafasi ya 8 akitumia muda wa saa 1:26.03.

Kwa wanaume kutoka HYAC, Pascal Mombo alishika nafasi ya 4 akitumia muda wa saa 1:04.10, wengine ni Nyangero Patrick (1:04.48), Oswald Kahuruzi (1:05.07), Nelson Priva (1:05.38).

Katika Bagamoyo Historical Marathon 2014, mbio za kilometa 10 zilifanyika ambapo Joseph Sule (Jeshi la Magereza-Arusha) alishika nafasi ya kwanza akitumia muda wa dakika 30:37 akifuatiwa na Elibariki Buko (HYAC) aliyekimbia kwa muda wa dakika 30:41 

Nafasi ya tatu katika mbio hizo ilichukuliwa na Msanduki Mohammed (Arusha) akitumia muda wa dakika 30:45, Godfrey Peter (HYAC) alishika nafasi ya 5 akikimbia kwa muda wa dakika 30:50.

Kwa upande wa wanawake Celina Amosi (Arusha) alishika nafasi ya kwanza akitumia muda wa dakika 34:16.03, akifuatiwa na Grace Jackson (Bagamoyo) akikimbia kwa dakika 36:20.13 na nafasi ya tatu akichukua Irene Chima (HYAC) kwa muda dakika 40:20.13

Mgeni rasmi wa mbio hizo Mkurugenzi Msaidizi wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Juliana Yassoda aliwataka wadau kujitokeza kwa wingi kudhamini mchezo huo katika maeneo mbalimbali nchini, na sio kujikita mjini kwani serikali ipo bega kwa bega na watanzania kuufanya mchezo wa riadha kurudi katika hadhi yake.

Aidha Dominic Mosha ambaye ni Mratibu wa Bagamoyo Historical Marathon 2014 aliwapongeza washiriki wa mbio hizo walivyojitokeza kwa wingi na kuwataka mwaka ujao kujitokeza kwa wingi kutetea rekodi zao.

Wanariadha wapatao 400 walishiriki kwa mara ya kwanza katika mbio hizo ambazo zitakuwa zikifanyika kila Jumapili ya kwanza ya mwezi Julai kila mwaka katika mji wa kihistoria wa Bagamoyo.



PREVIOUS STORY

No comments:

Post a Comment