HYAC

Attack with Style, Defend with Heart

Monday 23 June 2014

KONA YA PRO: JUNI 2014, BIOGRAPHY CHAMBER



 

 Suleiman Nyambui

Personal information
Born
February 13, 1953 (age 61)
Majita Musoma, Tanzania
Sport
Country
Sport
Event(s)
College team
Achievements and titles
Personal best(s)
1500 metres: 3:35.8[1]
Mile: 3:51.94[1]
Indoor 2-mile: 8:17.9[1]
5000 metres: 13:12.29[1]
10,000 metres: 27:51.73[1]
Marathon: 2:09:52[1]
Medal record[hide]
Competitor for  Tanzania
Silver
Bronze
5,000 metres
Suleiman Nyambui alizaliwa Februari Mosi, 1953 Majita, Musoma nchini Tanzania.

Huyu ni mwanariadha nchini Tanzania ambaye alijikita katika mbio fupi na ndefu katika maisha yake ya riadha. Kwa sasa ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la Riadha nchini Tanzania (AFT).

Alitwaa Medali ya Shaba katika All Africa Games 1978, medali ya Fedha katika Mbio za Mita 5000 kwenye Michuano ya Olimpiki 1980 na alishika nafasi ya kwanza katika marathon kwa miaka 3 mfululizo kati ya mwaka 1987 na 1988. Na ana rekodi nyingi katika mashindano ya ndani ya nchi.

Nyambui na Riadha
Nyambui aliachwa mpweke baada ya kumaliza elimu ya msingi, hivyo akaanza kuwa mvuvi katika wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza. 

Alipokuwa Mwanza alipata kuonekana kuwa ana kipaji cha kukimbia ndipo Chama cha Riadha cha Mkoa wa Mwanza kilipompa mafunzo  na vifaa ambavyo vilimwezesha kupanda hadi kufikia medani ya kimataifa.

Alijiunga na Jeshi la Kujenga Taifa na baadaye akiwa mwalimu katika Shule ya Bukumbi iliyoko kilometa 20 kutoka Jijini Mwanza alipata nafasi ya kwenda kusoma nchini Marekani ambako alisomea Shahada na Uzamili katika Chuo Kikuu cha Texas, El Paso (UTEP).

Aliwahi kupata nafasi ya kufundisha wanariadha wa nchini Saudi Arabia kwa mkataba na baadaye aliamua kurudi nyumbani Tanzania.

Akiwa nchini Marekani
Nyambui alikuwa akisoma nchini Marekani kati ya mwaka 1978 hadi 1982. UTEP alihitimu akiwa na umri wa miaka 29, akiwa na mataji 4 ya NCAA katika mbio za mita 10,000 akiweka rekodi ya kuwa mwanariadha wa kwanza  katika watano wa daraja la 1 kwa wanaume kupata mataji manne mfululizo.

Pia alishinda mataji 3 mfululizo ya NCAA ya mita 5,000 akiwa UTEP na alikuwa Bingwa wa Mbio za Nyika NCAA 1980.

Kubwa zaidi lililovutia ni katika Michuano ya Millrose (Millrose Games) Jijini New York Februari 1981, Suleiman Nyambui alivunja rekodi ya dunia ya mita 5000, akikimbia kwa dakika 13:20.4 akimwaacha Alberto Salazar ambaye alivunja rekodi ya mita 5000 kwa nchini Marekani.  

Baada ya Masomo UTEP
Nyambui aliiwakilisha Tanzania katika Michezo ya Olimpiki kwa wanaume mita 5,000 mwaka 1980 ambapo, alimaliza wa pili akitanguliwa na Miruts Yifter.

Baada ya hapo alikimbia mbio fupi na baadaye akatuama katika mbio ndefu.

Alishinda mara mbili mfululizo Berlin Marathon Oktoba 4, 1987 akitumia muda wa saa 2:11:11; Oktoba 9, 1988 alishinda mbio hizo akikimbia kwa saa 2:11:45 pia mwaka 1988 alitwaa taji la Stockholm Marathon 

ILIYOPITA BOFYA KIUNGO HIKI
Imetayarishwa na:
Jabir Johnson, Afisa Habari na Mawasiliano
Holili Youth Athletics Club (HYAC)
Mei 2014.

No comments:

Post a Comment