HYAC

Attack with Style, Defend with Heart

Friday 6 December 2013

FURAHA SAMBEKE, NEEMA MATHIAS WATISHA SERENGETI MARATHON KILOMETA 21



W
anariadha Furaha Sambeke na Neema Mathias , wa Holili Youth Athletics Club wameiwakilisha vyema kabla hiyo katika mbio za Pili za Serengeti Marathon mwaka 2013 baada ya kushika nafasi za pili na tatu kwa upande wa Wanawake.
 
FURAHA SAMBEKE AKIPOKEA MEDALI NA MKUU WA MKOA SIMIYU PASCAL MABITI
NEEMA MATHIAS AKIPOKEA MKONO WA PONGEZI NA MHESHIMIWA TITUS KAMANI MBUNGE WA BUSEGA

Wanariadha hao wa kike walikimbia mbio za kilometa 21 (Half Marathon) wakiachwa na mkongwe Mary Naali wa mkoani Arusha kwa dakika 10.

Mbio hizo ambazo zilianza mapema majira ya saa moja asubuhi ya Desemba 4, mwaka huu katikati ya Hifadhi ya Wanyama ya Serengeti karibu na geti la Ndabaka wilayani Bunda mkoani Mara kwa wafukuza upepo kutoka ndani na nje ya Tanzania.

Mary Naali alimaliza mbio hiyo katika kijiji cha Lukungu, kilichopo Lamadi wilayani Busega Mkoani Mwanza kwa kutumia muda wa 1:16:45.

Furaha Sambeke alimaliza mbio hizo kwa muda wa 1:26:24 wakati Neema Mathias alihitimisha safari yake kwa muda wa 1:30:23.

Washindi wengine katika mbio hizo walikuwa  Magret  Gilbert kutoka Urambo Tabora aliyekimbia kwa muda wa 1:35:02 akifuatiwa  na Anna Kabote alifunga nafasi tano bora kwa muda wa 1:35:54

IN BRIEF:
SERENGETI MARATHON 2013
Kilometa 21

NAFASI
JINA
MUDA
ANAKOTOKA
1.
Mary Naali
1:16:45
Arumeru - Arusha
2.
Furaha Sambeke
1:26:24
Holili Youth Athletics Club
3.
Neema Mathias
1:30:23
Holili Youth Athletics Club
4.
Magreth Gilbert
1:35:02
Urambo - Tabora
5.
Anna Kabote
1:35:54
Busega -Simiyu
·         PICHA ZAIDI KUHUSU SERENGETI MARATHON ZITAKUJIA BAADAYE

No comments:

Post a Comment